ZIJUE SABABU 5 ZINAZOMFANYA MWANAMKE KUTOKWA NA DAMU UKENI BAADA YA TENDO LA NDOA
Kuna sababu nyingi kwa nini mwanamke anaweza kuvuja damu baada ya kufanya tendo la ndoa. Tatizo Hili kitaalamu tunaita "postcoital bleeding
Iwapo una wasiwasi kwa sababu unatokwa na damu ukeni baada ya kufanya tendo la ndoa, tafuta ushauri kutoka kwa daktari wa magonjwa ya uzazi. Watakuuliza kuhusu historia yako ya matibabu na kutathmini dalili zako. Kisha wanaweza kukushauri ikiwa matibabu yoyote yanahitajika.
Je, Nini Husababisha Tatizo Hili?
Zipo sababu nyingi zinazomfanya mwanamke kutokwa na damu ukeni baada ya tendo la ndoa, lakini nitakupa tano tu hapo chini, nazo ni:
π. Maambukizi ukeni kama vile PID au magonjwa ya zinaa kama vile pangusa.
π. Uke kuwa mkavu kutokana na mvurugiko wa homoni
π. Michubuko ukeni kutokana na misuguano wakati wa kushiriki tendo la ndoa
π. Kuvimba kwa mlango wa kizazi
π. Saratani kwenye mji wa mimba.
Je, Vipimo Vinafanyikaje?
Kulingana na dalili zingine zozote na historia yako ya matibabu, daktari anaweza kupendekeza vipimo au uchunguzi fulani, kama vile:
π. Kipimo cha ujauzito
π. Kipimo cha nyonga kwa kuingiza kidole ukeni
π. Kutazama mlango wa kizazi kwa kutumia kifaa kiitwacho speculum
Je, Nini Humfanya Mwanamke Kuhisi Maumivu Wakati Wa Tendo La ndoa?
Wanawake wanaweza kupata maumivu wakati au baada ya kushiriki tendo la ndoa, ama kwenye uke au ndani ya nyonga kabisa.
Maumivu katika uke yanaweza kusababishwa na:
π. Maambukizi ya zinaa kama vile kisonono, au pangusa (PID)
π. Mvurugiko Wa homoni na kusababisha uke kuwa mkavu
π. Kutokuwa na hisia au hamu ya tendo la ndoa
π. Misuli ya uke kubana,
π. Kuvimba kwa fibroid karibu na mlango wa kizazi
Je, Suluhisho Lake Ni Nini?
Azmoh Herbal tunazo dawa nzuri kabisa zenye uwezo mkubwa wa kuondoa Vyanzo Vyake
Maoni