TABIA 12 ZITAKAZOKUFANYA UWE MWENYE FURAHA MAISHANI



 TABIA 12    ZITAKAZOKUFANYA     UWE     MWENYE    FURAHA     MAISHANI


1.    Samehee 

hata wasiostahili kusamehewa.

Usikubali kuwa na kinyongo au ugomvi na mtu yeyeto. 

Jifunze kupotezea. 

Usimjibu kila mtu kila kitu. 

Hata ukimya ni majibu. 


 2.   Jiamini

Hakuna lisilowezekana chini ya jua. Anza sasa.

Wenye imani wana amani kila wakati. 

Wenye imani wanakuwa na uhakika wa kile wanachokitarajia. 


 3.   Jifunze 

Mungu hakumuumba mtu kuweza kila kitu wakati wowote. 


 4.   Jipende

Umeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Usijidharau wala kujishusha kiwango. Jitamkia mambo mazuri kila wakati.


 5.   Tabasamu

Furaha ni tiba ya moyo

Jifunze kuhesabu baraka ambazo Mungu amekupatia itakisaidia kutabasamu kila wakati.


 6.   Usihukumu

Hakuna mwaminifu chini ya jua. Kila mmoja anakosea hata wewe huwa unakosea na kuwakosea wengine. 


 7.   Jiheshimu

Mfumo wa maisha yako ndio utakuwa msaada kwa wengine. Wewe ndiye utakayewafanya wengine kukutafasiri.


 8.   Panga malengo

Malengo ni taa, dira, ramani,kesho, mwelekeo, matumaini. Usiishi pasipo kujua kesho yako au pasipo kujua unapoelekea.


 9.   Fanya Ibada

Mahusiano yako pamoja na Mungu ndio chanzo cha kubarikiwa kwako.


 10. Kula vizuri

Mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu kuwa makini sana kwenye ulaji wako. Usile chochote unachotaka Bali kula chochote kinachohitajika mwilini mwako. 


 11. Kuwa mkarimu

Hukuja duniani na kitu Bali vyote ulivyonavyo chanzo chake ni Mungu. Lakini pia vyote utaviacha duniani siku yako ya kufa itakapofika. Ukarimu ni akiba ya baadae kwa ajili yako na kizazi chako.


 12. Kuwa mwenye shukrani

Ukitambua na kutafakari ulipotolewa na huyu Mungu hakika hautashindwa kusema asante kwake. 

Mshukuru Mungu kwa kila jambo hata kama mengine yanaenda vibaya endelea kumwambia Mungu asante.

Maoni