UJASIRIAMALILI

Mjasiriamali ni mtu mwenye uthubutu, asiyeogopa kushindwa
na mwenye maamuzi binafsi ambaye ameamua kuingia kufanya
kazi halali inayomuingizia kipato chake binafsi kwa kutumia
ujuzi wake, fedha zake, utaalamu wake n.k. Ni mtu mwenye upeo
wa kuona nafasi (fursa) haraka na kuitumia. Huyu mara zote
hufananishwa na mchezaji ambaye hapotezi nafasi anayoipata.
Kifupi ni mtu wa maamuzi na uthubutu bila kusubiri.
Mtu huyu hana tabia ya kugeuka nyuma na kuangalia alipotoka,
au nini watu wanasema kumkatisha tamaa, lakini yeye huangalia
kesho yake itakavyokuwa nzuri, kuliko leo yake ambayo watu
wanambeza na kumkatisha tamaa juu ya wazo alilonalo.

Sifa za mjasiriamali

Mjasiriamali huwa ana sifa za kipekee zinazomtofautisha na
mwingine. Habari njema ni kuwa sifa hizi hatuzaliwi nazo. Sifa
hizi tunazitengeneza wenyewe kwa kwa kujifunza kupitia vyanzo
mbalimbali.Zifuatazo ni baadhi ya sifa za Mjasiriamali;


                     


                  1. Mjasiriamali ni kiongozi

Walimu wengi wamekuwa hawafundishi hii kama sifa ya
mjasiriamali lakini hii ni moja ya sifa muhimu anayopaswa kuwa
nayo mjasiriamali. Mjasiriamali kwanza lazima awe kiongozi wa
maisha yake. Ajue kujisimamia mwenyewe na kusimamia mambo
yake yeye kama yeye bila kusubiri mtu kutoka nje. Mjasiriamali
ni lazima ajue kuiongoza biashara yake lakini hasa kuwaongoza
watu anaofanya nao kazi kama wapo.

2. Mjasiriamali ni mwenye uwezo wa kufanya maamuzi
binafsi

Mtu yeyote mwenye sifa ya kuwa mjasiriamali ni lazima awe
na sifa hii ya kuwa na maamuzi katika maeneo mbalimbali hasa Mwongozo wa Biashara
maamuzi juu ya jambo fulani ambalo analiona kwake lina faida.
Ni mtu asiyechelea kutumia kila fursa anayoiona.

3. Mjasiriamali ni mtu mwenye bidii (Anayejituma)
Mjasiriamali ni lazima awe ni mtu anayejituma na ambaye
ameachana kabisa na tabia ya uvivu. Kwake yeye kufanya kazi
kwa bidii ni sehemu ya maisha yake na anafahamu vyema kuwa
kama akilala hata ujasiriamali wake utalala pia.

4. Mjasiriamali ni mtu asiyekata tamaa
Ni lazima mjasiriamali yeyote awe na moyo wa kutokata tamaa
hata kama anapitia katika changamoto gani. Ni mtu anayeangalia
mbele tu na hata hafikirii juu ya changamoto na maneno ya
kukukatisha tamaa ya watu. Kwake yeye changamoto humpa
kujifunza na kuendelea kuwa bora kwa kila anachokifanya.

5. Mjasiriamali ni mtu anayetumia kile alichonacho
mkononi
Mjasiriamali ni lazima awe mtu wa kutumia kile alichonacho
mkononi. Mjasiriamali huwa hasubiri mtaji wa laki moja wakati
ana elfu thelathini mkononi. Hufikiri namna ya kutumia elfu
thelathini wakati akisubiri mtaji wa shillingi elfu hamsini.

6. Mjasiriamali ni mwenye kiu ya ndani ya kufanikiwa
Mjasiriamali ni lazima awe na msukumo wa ndani wa kuona
kuwa atafanikiwa kwa chochote anachokifanya. Msukumo
huu ndio humfanya kuamka mapema na kufanya vile anaweza
kufanya bila kuangalia wanaomkatisha tamaa.

7. Mjasiriamali ni mbunifu
Mjasirimali ni lazima aweza kufanya kwa utofauti na kuleta vitu
vipya ili kuongeza tija katika kile anachokifanya. Mjasiriamali ni
lazima awe na uwezo wa kujiongeza na kuonesha utofauti katika
kile anachokifanya.


8. Mjasiriamali ni mgunduzi
Mjasiriamali ni mtu anayepaswa kufanya vitu vipya ambavyo
havijawahi kutokea. Ni mtu anayetumia muda mwingi kutafuta
vitu ambavyo havijawahi kutokea

HIVI NI BAADHI MINGONI MWA VITU UNAVYOTAKIWA KUFAHAMU KUHUSU UJASIRIAMALI.

Maoni